Psalms 120

Kuomba Msaada

Wimbo wa kwenda juu.

1 aKatika dhiki yangu namwita Bwana,
naye hunijibu.
2 bEe Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo
na ndimi za udanganyifu.

3Atakufanyia nini,
au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
4 cAtakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa,
kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.

5 dOle wangu kwa kuwa naishi Mesheki,
kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
6Nimeishi muda mrefu mno
miongoni mwa wale wanaochukia amani.
7Mimi ni mtu wa amani;
lakini ninaposema, wao wanataka vita.
Copyright information for SwhNEN